Raia hadi 150 waliuliwa katika shambulizi la kutokea angani Machi 17 katika kitongoji cha al-Jadida mjini Mosul.
Shirika hilo limesema agizo la maafisa wa Iraq lina maana vikosi vya muungano vilitakiwa kufahamu idadi kubwa ya raia wangekuwa wahanga wa mashambulizi yoyote ya kutokea angani.
Shirika la Amnesty International linasema kushindwa kuyazuia mashambulizi hayo huenda kumevunja sheria za kimataifa. Maafisa wa Marekani na Iraq wanachunguza shambulizi hilo pamoja na mengine.
0 Comment to "Amnesty: Mashambulizi ya Mosul ni kinyume na sheria"
Post a Comment